Jinsi ya Kupakua DJ Mixes Kali za Mdundo Kupitia Mtandao wa Vodacom

Kampuni ya kutitirisha muziki ya Mdundo imeshirikiana na Vodacom Tanzania kuzindua huduma mpya kwa wateja wa Vodacom itakayo waruhusu kupakua mixes kali kutoka kwa maDJ tajika nchini Tanzania.

Kupitia ushirikiano huo, wateja wa Vadacom wantaweza kupata mixes kutoka kwa DJ Summer, DJ AllyBi, DJ YLB, DJ Ferruh, DJ Bike na DJ Massu; kwa kuanzia Tsh 80 kila siku.

Mixes mpya zinapatikana kila siku, zikijumuisha nyimbo mpya za Bongo Flava, Naija, Gospel, Taarab, Reggae na HipHop.

Kupata mixes hizo, unaweza kutembelea mdundo.com/djmixes kupakua mix ya DJ unayemkubali zaidi.

Kwa wateja wa Vodacom, unaweza kupata mixes kwa kubonyeza *149*01# na kufuata masharti na vigezo zilizotolewa.

Pia, unaweza ingia kwa Playstore na kupakaua Mdundo App au My Vodacom App na kufuata vigezo zilizotolewa ili kupata mixes hizo.

Mixes hizo ni za kipekee kwa watumiaji wa Mdundo.com na wateja wa Vodacom. 

Vigezo na masharti, kuzingatiwa. Kwa taarifa zaidi, tembelea mdundoforfans.com

Leave your comment