Video 5 Moto Zinazotamba Kwenye Mtandao wa YouTube Tanzania

[Photo Credit:Zuchu Instagram]

By Branice Nafula

Follow Us on Google News

Wasanii wengi nchini Tanzania wanaendelea kutoa nyimbo mpya kila kukicha.

Wiki hii, video kadhaa zimevuma mitandaoni na kupata kutazamwa na watu wengi.

Baadhi ya video zilizofanya vizuri kwenye mtandao wa YouTube wiki hii ni:

Nobody- Zuchu akimshirikisha Joeboy

‘Nobody’ ni wimbo wa kimapenzi ambapo Zuchu anamhakikishia Joeboy kuwa hamna anayempenda kama yeye, na kwa upande wake Joeboy anamhakikishia mapenzi ya dhati. Wiki moja baada ya kuachiliwa, wimbo huu unawatazamaji zaidi ya millioni mbili nukta tatu kwenye mtandao wa YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=04Roh3SDyN0&ab_channel=Zuchu

Litawachoma – Zuchu na Diamond

Wimbo huu umetazamwa zaidi ya mara milioni mbili kwenye YouTube chini ya wiki mbili. ‘Litawachoma’ ndio wimbo wa kwanza ambao Zuchu amemshirikisha mkuu wake Diamond Platnumz.

https://www.youtube.com/watch?v=g9spgkHS2bs&ab_channel=Zuchu

Download Diamond Music for Free on Mdundo

Do me - Nandy akimshirikisha Bilnass

‘Do me’ ni wimbo mzuri wa mapenzi kwa wanandoa wanaoelezea mapenzi yao kwa kila mmoja. Ukisikiliza toleo hili jipya, unahisi kuwa wasanii wote wanazungumza kutoka kwa mioyo yao kwani mapenzi yao ni ya kweli kisanii na katika maisha halisi. Kufikia sasa wimbo huu wa Bilnass na Nandy umepata watazamaji zaidi ya milioni moja.

https://www.youtube.com/watch?v=enz1B5PuUac&ab_channel=Nandy-TheAfricanPrincess

Far away – Country wizzy akimshirikisha Harmonize

‘Far away’ ni wimbo wa mapenzi ambapo Country Boy anaangazia namna mpenzi wake anavyomfurahisha. Kufikia sasa wimbo huu wa Harmonize na Country Wizzy una watazamaji zaidi ya laki tano.

https://www.youtube.com/watch?v=dtpARfzLvIc&ab_channel=CountryWizzy

Haunisumbui - Diamond Platnumz

“Haunisumbui” ni wimbo wake Diamond akisimulia hadithi ya mpenzi wake wa kitambo ambaye amekuwa akimsumbua kwa muda baada ya mapenzi yao kuvunjika. Kulingana na Diamond, yule wa zamani hapaswi kuingilia maisha yake tena, kwani yote anayofanya kwa sasa hayamsumbui kamwe. Kwa sasa ni wimbo aina ya audio tu na umetazamwa zaidi ya mara milioni moj nukta saba.

https://www.youtube.com/watch?v=BgI4x51X8WU&ab_channel=DiamondPlatnumz

Leave your comment