Nyimbo 5 Kali Zinazovuma Bongo Wiki Hii

[Anwani ya Picha: The Citizen]

Mwandishi Omondi Otieno

Tufuate Kwenye Google News

Wasanii wengi nchi wanajitahidi kutoa nyimbo mpya na kuanda tamasha kila wikendi ili kurudisha pesa walizopoteza miezi kadhaa iliypopita baada ya janaga la corona kusitiza mikutano mikubwa.

Wki hii, video kadhaa zimevuma mitandaoni na kupata kutazamwa na watu wengi. Baadhi ya video zilizofanya vizuri ni:

Litawachoma – Zuchu na Diamond

Wimbo huu umetazamwa zaidi ya mara milioni mbili kwenye YouTube chini ya wiki mbili. ‘Litawachoma’ ndio wimbo wa kwanza ambayo Zuchu amemshirikisha mkuu wake Diamond Platnumz.

https://www.youtube.com/watch?v=B-AtdyO1DZA

Wasted Energy – Alicia Keys na Diamond

Wimbo huu ni moja wapo ya nyimbo kutoka kwa albamu mpya ya Alicia Keys iitwayo ‘Alicia’. ‘Wasted Energy’ imetazamwa zaidi ya mara elfu mia tisa kwenye YouTube katika mda wa siku nne. Wimbo huu umezua utata nchi hasa kwa wafuasi wa Diamond ambao waligadhabishwa sana nayeye kupewa sekundi 26 pekee yake.

https://www.youtube.com/watch?v=f_laxGbqL4I

Ongeza – Diamond

Diamond aliachilia wimbo huu wikendi iliyopita. Kwa sasa, video yake bado haijaachiliwa. Kwenye mtandao wa YouTube, ‘Ongeza’ imetazamwa mara elfu mia nane kwa mda wa siku nne.

https://www.youtube.com/watch?v=-AX3WTAmJno

Sexy Mama – Lava Lava na RJ The DJ

Video hii ni mohja wapo kati ya nyimbo kutoka kwa albamu yake Romy Jons iitwayo ‘Changes’. Video hii iliachili wiki moja iliyopita na imetazwa zaidi ya mara milioni moja kwwenye YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=_lv3zr_Ql7s

Cheche – Zuchu na Diamond

Video ya wimbo hii imefutwa kwenye YouTube lakini toleo lisilokuwa na video bado lipo. Toleo hilo la ‘Cheche’ limetazamwa zaidi ya mara mia tisi kwenye YouTube.

https://www.youtube.com/watch?v=f5etClN9o6Q

Unapotazama nyimbo hizi zote, kile kinajitokeza ni kuwa kwa njia moja ama nyingine, zote zina uhusiano na lebo ya Wasafi chini ya uongozi wake Diamond Platnumz.

 

 

Leave your comment