Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Vanessa Mdee Baada Ya Money Mondays, ‘Ningependa Usikiliza Albamu Ya Grace Matata’
8 May 2018

Msanii Vanessa Mdee baada ya kuachia albamu yake ya kwanza Money Mondays amesema angependa kusikiliza albamu mpya kutoka kwa Grace Matata kwa sasa.
Muimbaji huyo wa ngoma ‘Wet’ amesema kuwa amekuwa akifuatilia muziki wa Grace Matata na umekuwa wenye kumvutia hivyo angependa kuupata ukiwa katika albamu (package).
“Nilikuwa nasikiliza kazi za Grace Matata juzi kati, ladha zake ni tofauti sana, ningependa kusikiliza albamu nzima kutoka kwake ana kitu fula hivi akikuimbia na gitaa unatulia,” Vanessa ameiambia Clouds TV.
Utakumbuka kuwa Grace Matata alishatoa albamu yake ya kwanza iliyokuwa inakwenda kwa jina la Nyakati.
Muimbaji huyo amemtaja Maua Sama kama msanii mwingine ambaye angependa kusikiliza albamu kutoka kwake. Pia Vanessa Mdee ameeleza kuwa EP ya Mimi Mars itatoka mwisho mwa mwaka huu ikiwa na nyimbo sita.
Courtesy: bongo5.com
Weekly Top 10 songs

BIkola2:58
KAPEKE LONDON2:23
In My Bed2:50
Buwooma2:44
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Paver2:55
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
CHAMPION GAL3:00
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Joy Is Coming3:08
Top stories
- Daniel Sifuna
14 May
- UPCOMING EP FROM EMKAY64
14 May
- Generation
16 May
- NEW SONG ALERT
16 May


Leave your comment