TANZANIA: Joh Makini na Davido Washoot Video ya Collabo Yao

Hatimaye Joh Makini na Davido wamefanikiwa kushoot video ya collabo yao.

Video hiyo imefanyika jijini Johannesburg, Afrika Kusini. Kupitia Instagram ni Davido ndiye aliyetoa habari hizo njema kwa kuweka picha akiwa na Joh pamoja na warembo sita.

“Back to work !! On set  shoot @johmakinitz ft Davido ….. TZ  x NAIJA,” ameandika.

Wimbo huo una takriban mwaka na nusu tangu urekodiwe na ni video pekee iliyokuwa inasubiriwa ili uachiwe rasmi.

Source: bongo5.com

Leave your comment