TANZANIA: Fid Q Amaliza Utata Kati Yake na Joh Makini

Msanii Fid Q amesema anashangazwa na baadhi ya watu wanaomuandika vibaya katika mitandao ya kijamii kuwa ana 'bifu' na Joh Makini kutoka Weusi hali ya kwamba hawana tofauti yoyote baina yao. 

Kubanda alifunguka zaidi kwa kusema hajawahi hata kuwaza kugombana na 'rappa' huyo mwenye 'hit song' inayojulikana kwa jina la waya.

“Unajua hata mimi nilikuwa nazipokea tu hizo 'story' kama wanavyopokea watu wengine maana sijawahi kuwa na shida na jamaa, kawaida ya wabongo huwa tunatafuta 'challenger' kama mtu mpya akiingia kwenye game so Joh alitumiwa kama 'challenger' wangu maana mimi nafanya vizuri tangu back then”. Alisema Fid Q

Aidha msanii huyo amesema njia ya muziki na kibinadamu hana kinyongo wala ugomvi pia aliendelea kusisitizia kuwa yeye ndiye aliyemuunganisha Joh katika 'project' ya nje kwenda kufanya kazi japokuwa muhusika mwenyewe atakuwa hatambui hilo.

Source: eatv.tv

Leave your comment