TANZANIA: Mzee Yusuf kwa sasa yupo katika biashara zaidi kuliko muziki - Amigo

 

 

Mmoja kati ya wasanii wa Mzee Yusuph Amigo amesema Mzee Yusuf ni mtu ambaye kwa sasa yupo katika biashara zaidi kuliko muziki na kuwaachia nafasi wao wajulikane.

Akizungumza ndani ya eNews Amigo amesema “kwa kweli sifahamu na sijataka kuingia kiundani zaidi kuwa nini kinamsumbua mimi ninachofikiria ni kwamba nafanyaje nini ili baba yangu huko aliko apate faraja kwamba mimi sipo kazini kutokana na majukumu yangu binafsi lakini mtoto wangu anafanya kazi na taarifa nazipata”

Alimalizia kwa kusema “Na yule ni mtu mkubwa sasa ana familia mbili ana kampuni amefungua ana vitu vingi vya kufanya naamini ni wakati wa yeye kusema kuna vitu sasa ngoja niviweke sawa kwa kuwa kuna wakati alienda china akarudi ameamua kuwekeza sana katika biashara kuliko kwenye muziki”

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

 

Leave your comment