TANZANIA: Rappa One The Incredible aja na movie ya ‘Bongo Na Flava’

 

Filamu mpya ‘BongoNaFlava’ ya rappa One The Incredible imeonyeshwa kwa mara ya kwanza katika ukumbi wa Goeth-Institut Upanga jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali. Filamu hiyo kuwakutanisha mastaa wa muziki kama Fid Q, Wakazi, Makamua, Lamar pamoja na washiriki wengine.

Kupitia ukurasa wa instagram, One aliandika: Firstviewing at Goeth e Institut – Upanga, this Thursday. Hii ndio mara yangu ya kwanza kama muigizaji… Karibu Goethe Institut – Upanga, alhamisi hii uione filamu ya #BongoNaFlava iliyotayarishwa chini ya usimamizi wa director nguli @rrahc itaoneshwa kwa mara ya kwanza. #Pichakubwa

One The Incredible

 

Malle Hanzi ni mmoja kati wa watu walio shuhudia tukio hilo, naye aliamua kuandika uchambuzi wa filamu hiyo.

Dhumuni la kuanzishwa kwa taasisi hii ni kusambaza/kufundisha utamaduni wa kijerumani na pia kubadilishana tamaduni na mataifa mengine kupitia filamu, muziki, fasihi n.k

Jioni ya Tarehe hiyo katika “Thieta” ya taasisi hiyo kulikuwa na filamu iitwayo “Bongo na Flava” iliyokuwa ikioneshwa kwa mara ya kwanza. Habari njema ni kwamba inaweza ikaoneshwa tena katika tamasha la ziff mwaka huu. Katika filamu hii imehusisha wahusika kama One the Incredible, Fid Q, Wakazi, Cheusi (wa siri ya mtungi), Lamar, Songa, Makamua, Salu T, Saigon na wengineo huku ikiwa imetayarishwa na kuongozwa na RlahC, Karabani na wengineo.

Kusema ukweli ni Filamu nzuri sana inayosadifu sanaa na maisha ya kila siku. Watayarishaji na waigizaji wa Filamu wamejitahidi sana katika kuikamilisha Filamu hii. Pongezi za moja kwa moja zimuendee One The Incredible ambaye ameigiza kama mhusika mkuu akifahamika kama Zopa. Kiukweli One kavaa uhusika ipasavyo; amefanya kazi nzuri sana.

Stori ya hii filamu inamhusu One (zopa) ambaye ni kijana aliyetoka kijijini mkoani kigoma na kwenda jijini Dar es salaam baada kuambiwa na rafiki yake kwamba kuna kazi atampatia. One anapofika jijini Dar es salaam anapatafuta anapokaa rafiki yake na kupapata lakini mama yake na rafikiye anamuambia rafiki yake yuko jela kwa kesi ya mihadarati. One anaomba hifadhi ya muda mfupi lakini anakataliwa na kufukuzwa.

One anaingia mtaani akiwa hajui anaanzia wapi anaishia wapi? Ndipo anajikuta analala katika vibaraza vya nyumba za watu na mwisho kabisa anavamiwa na vibaka na kuibiwa kila kitu. Baada ya kuhangaika hangaika ndipo anakutana na Makamua anayeamua kumpa hifadhi katika Ghetto lake na hapo ndipo muvi inapoanza. One anajikuta akifanya kila aina ya kazi ili kuwa na maisha mazuri na kuwa msanii mkubwa.

Jina la filamu BONGO NA FLAVA ndilo limetumiwa na waandaaji kuinadi filamu hii. Bongo inaweza kuwa na maana zaidi ya moja; baadhi ya maana ni 1. Bongo humaanisha Akili na 2. Bongo humaanisha Tanzania n.k. Neno flava (Flavor) tafsiri yake ni Ladha. Sina hakika kama wenye hii filamu walitaka kumaanisha Akili na Ladha au Tanzania na Ladha.

Kwenye filamu hii kuna mahali One alifika studio ya prodyuza mmoja akakutana na mlinzi ambaye alianza kumuita kwa jina la Bongo Fleva. Baadaye alimuuliza (Nukuu isiyo rasmi) “wewe ni bongo fleva?” One akasema “Unaweza kusema hivyo” yule mlinzi akarudia kumuuliza tena “Kwa hiyo wewe ni Bongo Fleva” One akajibu tena “Mimi nafanya Muziki”.

Kwa upande wa mmoja nilichokiona katika kipande hiko ni kushindwa kujiamini kwa One inawezekana pia alichanganya Maelekezo ya Scene inavyotaka na Imani yake binafsi. Jibu lake la kwanza ni kama alikubali yeye ni Bongo Fleva na jibu la pili ni kama alijaribu kuikataa kiaina.

Kwa upande mwingine inawezekana pia One aliamua kujivika uhusika wa Baadhi ya wana Hip Hop ambao akiwa na Wanahip hop anasema mwanahiphop na kuiponda Bongo Fleva na akiwa na wanabongo fleva anaenda nao sawa kwamba Bongo Fleva na Hip Hop ni kitu kimoja zote ni aina za muziki.

 

Leave your comment