TANZANIA: Alikiba asaini mkataba na ‘Sony Music’

 

Alikiba baada ya kusaini mkataba huo amewashukuru mashabiki wake kwa support waliompa toka aliporudi na wimbo wake wa 'Mwana' mpaka leo hii na kusema atafanya sherehe na mashabiki zake ili kufurahi nao baada ya kuweza kusaini mkataba na 'Sony Music'

 

 

"Nataka kukumbuka nilivyorudi kwenye game 2014 toka nimepumzika, nimepiga hatua kubwa sana na hii ni kutokana na support kutoka kwa mashabiki, mtanisamehe mashabiki pale nilipokosea, ila kwa furaha niliyonayo leo kusaini mkataba huu naomba nikirudi nifanye party ili nifurahi pamoja na mashabiki zangu ambao walikuwa na mimi mwanzo mpaka sasa" alisema Alikiba.

Mbali na hilo Alikiba amewashukuru waandishi wa habari na vyombo vya habari ambavyo vilikuwa vikimpa support kwenye kazi zake za muziki siku zote.

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

 

 

Leave your comment