TANZANIA: Ben Pol alikuwa anarap zamani - Stereo

 

 

Kama isingekuwa Stereo waliyesoma shule moja, kusingekuwa na hit single kama ‘Moyo Mashine za zingine.

“Ben alikuwa anarap,” Stereo ameiambia Bongo5.

“Sababu mimi nilianza hii michezo siku nyingi anakuja ananiambia ‘Stereo eeh hebu nisikilize’ namsikiliza. Lakini kuna siku alikuwa anaimba kitu nikamuambia ‘Ben rap is not your thing, unarap vizuri, una swag. Kipindi hicho cha akina Hajj Noorah, Chamber Squad ndio ilikuwa crew anayoipenda sana akina marehemu Mangwair (RIP), nikamuambia rap sio kitu chako wewe ni muimbaji,” anasema Stereo.

Anasema alimshauri Ben Pol kuwekeza nguvu zaidi kwenye kuimba na kutojali kama atachelewa kutoka.

“Ben Pol is there so I am proud of him,” ameongeza rapper huyo

 

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

 

Leave your comment