TANZANIA: Kajala akanusha kuwa na mahusiano na Msami

 

 

Msanii wa filamu Kajala Masanja amekanusha tetesi za kwenye mitandao ya kijamii kuwa anatoka kimapenzi na mkali wa wimbo ‘Mabawa’, Msami.

 

 

Mwingizaji huyo ambaye hivi karibuni ilisambaa video inayomuonyesha akidendeka na rapa Quick Rocka, ameiambia Clouds Fm kuwa Msami ni mshkaji wake wa karibu sana na sio mpenzi wake. “Unajua kuna watu wanaweza wakawa labda ni washikaji au wana vitu vingi pembeni lakini watu wengine hawajui, mi na Msami ni washkaji sana,” alisema Kajala.

Aliongeza, “Halafu sio kila siku watu watakuwa wanatuona barabarani au tunapostiana picha kwenye Instagram, lakini mimi na yeye tunaongea vitu vingi, kwa hiyo imekuwa rahisi mimi kuacha usingizi wangu kuja kwa Msami, sina uhusiano naye na vitu vingine mtavijua baadaye.”

Wawili hayo wamekuwa wakioneka wakiwa pamoja mara nyingi hali ambayo imeibua hisia huenda wakawa wanatoka kimapenzi.

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

Leave your comment