Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Wema Sepetu aonyesha uzalendo kwa kumuombea kura Diamond
30 May 2016

Baada ya hivi karibuni Alikiba kuwaomba watanzania wampigie kura Diamond anayewania tuzo za BET, Wema Sepetu naye amefanya hivyo.
Wema ametumia mtandao wa Instagram kuwaambia mashabiki wake wampigie kura ex wake huyo aliyetajwa kuwania kipengele cha Best International Act: Africa.
“Uzalendo ndo unaotakiwa… Tanzania Kwanza Vingine Baadae… Ama nene…? Vote Vote Vote….,” ameandika Wema kwenye picha ya BET Awards aliyoiweka Instagram.
Mashabiki wengi wamempongeza kwa uzalendo huo aliounesha licha ya yeye na Diamond kuwa mbali kwa sasa kutokana na kila mmoja kuwa na maisha yake. Wema na mpenzi wa sasa wa Diamond kuwa na tofauti
Diamond anachuana na mastaa wengine wa Afrika wakiwemo Wizkid, Yemi Alade, AKA, Cassper Nyovest na wengine wawili.
Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz
Weekly Top 10 songs
Top stories
- Brand new song
28 April
- So good EP release
28 April
- #NEW MUSIC #NEW artist #RAYMATS!
30 April




Leave your comment