TANZANIA: Sitaki maisha ya kiki, nataka kujenga jina langu kutokana na kazi zangu – Nuhu Mziwanda

 

Akizungumza kwenye kipindi cha 5SELEKT kinachorushwa na ting'a namba moja kwa vijana Nuh Mziwanda amesema kuwa kwa sasa yeye amefunga ukurasa wa mapenzi na Shilole hivyo hata ikitokea akataka kurudiana na yeye hawezi kufanya hivyo kwani ameshaanza maisha mapya ambayo anaona ni ya furaha zaidi.

Mbali na hilo Nuh Mziwanda ameeleza kuwa kwa sasa hataki tena maisha ya kiki na skendo alizoita kuwa ni za ajabu ajabu bali anataka kujenga jina lake kutokana na kazi zake kwenye muziki pamoja na kutengeneza muziki kama 'Producer'

 

 

Leave your comment