Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Raymond ana kila kitu ambacho msanii anatakiwa awe nacho - Madee
29 April 2016

Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, Madee amesema kuwa alitegemea kumuona Raymond akifanya vizuri, kutokana na jitihada alizokuwa nazo tangu akiwa Tip Top.

Madee
“Raymond yuko vizuri anafanya vizuri ni mtu ambaye nimekaa naye najua uwezo wake, ninachokiona nilikitarajia kwamba Raymond atakuwa mtu fulani, Raymond ana kila kitu ambacho msanii anatakiwa awe nacho, mara nyingi huwa naenda nae studio”, alisema Madee.
Pia Madee amezungumzia kuhusu suala la kufanya Hip Hop, na kusema kuwa kila mtu anafanya maisha anayoona yanamfaa, lakini iwapo atatokea mtu akimpa pesa nzuri atafanya Hip Hop.
“Hatulishani kila mtu anafanya maisha yake, ukiniambia mi nichane alafu kila siku unaniletea hela, baridi tu”, alisema Madee.
Weekly Top 10 songs
Top stories
- Jakabwana rmixx
14 June
- Approval
16 June
- Joe Chriss music
16 June




Leave your comment