Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Kuoa kwangu sio sababu ya kushuka kimuziki – Mr Blue
25 April 2016

Msanii huyo ameyasema hayo katika kipindi cha eNEWS kinachorushwa na kituo cha Eatv ambapo mtangazaji alimuuliza kuhusiana na yeye kuoa na haoni kwamba anaweza kushuka katika kazi zake za sanaa.
"Mimi siwezi kufeli kwenye muziki nimepata mitihani mingi kwenye muziki lakini sijashuka hadi leo, nimeanza muziki nikiwa mtoto na sasa hivi nimeshapata mtoto bado nipo kwenye muziki".

''Muziki ni kazi wapo wasanii wengi wa Marekani wameoa lakini wanafanya vizuri, kwa Tanzania mfano Mzee Yusuf ameoa mara mbili lakini sio kwamba ameshuka kwenye game kwa hiyo habari hizi siyo za kweli kabisa''- Amesisitiza Mr. Blue.
Mr. Blue amefunga ndoa hivi karibuni jijini Dar es salaam ambapo kwa sasa ana watoto wawili.
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Buwooma2:44
Joy Is Coming3:08
Nakupenda3:12
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Paver2:55
Ssirivawo ft yven feiz2:10
Ziyakuba kabotu6:57
Top stories
- #NEW MUSIC #NEW artist #RAYMATS!
30 April
- BABA FELA
30 April
- Nordman--Kelly yo collabo
30 April


Leave your comment