Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Baraka amvisha Naj pete
21 April 2016

Barakah Da Prince ambaye kwa sasa amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msanii wa kike, Naj, amedai kupiga hatua zaidi kuelekea kwenye uchumba.
Wamefunguka exclusively kwa Bongo5 kuhusu uhusiano wao:
“Yeah ni kweli mimi na Naj tuna uhusino na hadi kwetu nimeshamtambulisha na yeye kwao najulikana na pia nimemvisha pia pete, sio ya uchumba ila ni Promise Ring,” amesema Barakah.
“Ndio hivyo yaani kuna kazi pia ambazo tumefanya ila hazitatoka sasa hivi hadi kwanza kila mtu atoe single yake halafu ndio itakuja hiyo ngoma ya pamoja mimi na Naj,” ameongeza.
Kwa upande wake Naj amesema:
Ni kweli Barakah amenivisha pete kama alivyosema. Kwangu ni furaha sana maana nimeshakuwa na mahusiano yaliyopita lakini sikuwahi kufanya kitu kama hiki. Naona kabisa kuwa mahusino haya ni ya ukweli na naona kuna malengo kabisa, nafurahia kwakweli.”
“Bado hatujaanza kuishi wote ila muda mwingi tupo pamoja, nafurahia mahusiano yangu ya sasa. Ni kweli tumefanya ngoma ya pamoja lakini haitatoka sasa hivi mimi natakiwa niachie ngoma yangu na pia nishoot video, halafu pia nitarudi Uingereza mara moja, kuna vitu vyangu kule then nitarudi tena Bongo.”
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Buwooma2:44
Joy Is Coming3:08
Nakupenda3:12
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Paver2:55
Ssirivawo ft yven feiz2:10
Ziyakuba kabotu6:57
Top stories
- #NEW MUSIC #NEW artist #RAYMATS!
30 April
- Nordman--Kelly yo collabo
30 April
- One and only
01 May


Leave your comment