Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Juma Nature ampa onyo KR Mullah
8 April 2016

Mkongwe wa muziki Tanzania Juma Nature amempa onyo kali rapper KR Mulla baada ya kugundua kuwa ameanza kuroll na TID.Kwenye mahojiano ya mwisho kati ya KR Mulla na eNewz, KR alijitambulisha kama Raisi wa Radar Entertainment, ambayo inamilikiwa na TID, na siku za karibuni TID na KR wameonekana kuwa marafiki ukiachilia mbali kufanya kazi pamoja ndani ya Radar Entertainment.
Juma Nature ambaye aliwahi kufanya muziki ndani ya kundi la Wanaume Family pamoja na KR Muller ameamua kumpa onyo KR asije akashawishiwa na swahiba wake TID kuanza kutumia madawa ya kulevya yaani "Unga". kutokana na stori zilizozagaa mjini kumjumuisha TID kwenye orodha ya wasanii wanaotumia madawa ya kulevya. Zaidi Juma Nature alikataa kukubali kuwa KR ni Raisi wa Radar Entertainment kwa kuiambia eNewz kuwa "Hata huyo TID mwenyewe sio Rais, sasa KR ni Rais wa wapi? Rais ni Magufuli tu". Alisema Msitu wa Vina Juma Nature
Chanzo: Enewz
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Buwooma2:44
Joy Is Coming3:08
Nakupenda3:12
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Paver2:55
Ssirivawo ft yven feiz2:10
Ziyakuba kabotu6:57
Top stories
- One and only
01 May
- SHUKRANI
02 May
- Jaxon Ryker Official profile
30 April


Leave your comment