Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
TANZANIA: Mr Blue apata menejimenti mpya kutoka Afrika Kusini.
6 April 2016

Msanii wa muziki nchini Tanzania, Kherry Sameer Rajab a.k.a Mr Blue amedai kuwa amepata menejimenti mpya kutoka Afrika Kusini na ndiyo itakayomsimamia kazi zake.
Akizungumza katika kipindi cha XXL cha Clouds Fm, msanii huyo ammesema kwa sasa yuko na menejimenti mpya na wameshamtafutia kolabo na msanii mkubwa wa Afrika. “Kwakweli mwaka huku nashukuru nimeunza vizuri kwangu kwasababu kwanza nimepata menejimenti nzuri sana ambayo ipo ‘South Africa’, jamaa ni watanzania wanaoishi kule wameuona muziki wangu ni mzuri sema nimekosa ‘Kampani’ ya watu wakunisapoti kwahiyo wamejitolea kunisaidia na mwaka huuu nitafanya video kubwa na msanii mkubwa Afrika”, alisema Mr. Blue.
“Kwahiyo Mungu akinisaidia mwaka huu nitafanya video kubwa na msanii mkubwa Africa ambaye siaki kumtaja mapema. Kwahiyo wimbo utaandaliwa Afrika Kusini pamoja na video japokuwa kuna nyimbo kadhaa nimeshazirekodi nitazitoa kwanza halafu hiyo ya kimataifa itatoka katikati ya mwaka huu au mwishoni”, aliongeza Mr.Blue.
Chanzo: Bongo5
Weekly Top 10 songs

Kamwambie3:47
chile-one-so-lucky4:02
Buwooma2:44
Joy Is Coming3:08
Nakupenda3:12
Udede Ft Msomali x Malume & Samas Alifata Hela Remix6:34
Msaliti 11:25
Paver2:55
Ssirivawo ft yven feiz2:10
Ziyakuba kabotu6:57
Top stories
- One and only
01 May
- SHUKRANI
02 May
- Okello oyumu
01 May


Leave your comment