Exclusive DJ Mixes and 100% Ad-Free Music!
Zuchu Aungana Na Innos B Kwenye “Nani Remix”
2 June 2023

Picha: Instagram
Imeandikwa na Charles Maganga
Msanii nguli kutoka Tanzania, Zuchu kwa mara nyingine ameamua kukosha mashabiki zake baada ya kuachia remix ya wimbo wake wa “Nani” ambao amemshirikisha Innos B
Zuchu aliachia “Nani” takriban wiki 3 zilizopita kwa mapokezi makubwa ambapo mashabiki wengi wa muziki wameonekana kupenda ngoma hiyo ambayo imetayarishwa na producer S2kizzy
Kwenye “Nani Remix” Innos B ameongeza ladha ya kikongo kwenye mdundo huo ambapo pia amesikika akiimba kwa lugha ya Kikongo. Zuchu kwa upande wake, amekoleza “Nani Remix” na sauti yake mujarab pamoja na mashahiri mepesi yasiyochosha.
Hii si mara ya kwanza kwa Zuchu na Innos B kushirikiana kwenye ngoma ya pamoja. Miezi mitatu iliyopita wawili hao walikutana pamoja kwenye ngoma ya “Kiss” ya kwake Innos B.
Weekly Top 10 songs

In My Bed2:50
KAPEKE LONDON2:23
BIkola2:58
Buwooma2:44
Baddie remix feat Shannnon, aaronix, Tojo3:14
Paver2:55
Nitampeleka kwa Mama (ft. Xouh)3:44
Ex Nkubilako ft DonMusa2:55
CHAMPION GAL3:00
Kamwambie3:47
Top stories
- UPCOMING EP FROM EMKAY64
14 May
- Daniel Sifuna
14 May
- Generation
16 May
- NEW SONG ALERT
16 May


Leave your comment