NYIMBO ZINAZOTAMBA TANZANIA WIKI HII
2 June 2023
Picha Instagram
Imeandikwa na Charles Maganga
Kama ulikuwa unajiuliza ni ngoma gani ambazo zinafanya vizuri zaidi nchini Tanzania kwa wiki hii basi itoshe kusema kuwa makala hii ni kwa ajili yako.
Kutoka kwa wasanii ksma Mbosso, Nandy, Marioo na wengineo wengi hizi hapa ni ngoma tano zinazofanya vizuri zaidi Tanzania kwa wiki hii:
Amepotea - Mbosso
Amepotea ya Mbosso imeonesha ni kwa namna gani, msanii huyo kutokea WCB ana kipaji cha uandishi na bila shaka mashabiki wameipokea kwa mikono miwili ngoma hii ambayo kufikia sasa imeshatazamwa mara Milioni 2.9 tangu kuachiwa kwake
Tomorrow - Marioo
Linapokuja la Amapiano kwa lugha ya Kiswahili, fundi mara nyingi huwa ni mmoja tu, naye ni Marioo na kupitia mkwaju wake wa “Tomorrow” Marioo ameweza kuthibitisha hilo
Falling - Nandy
Video ya “Falling” ya kwake Nandy inastahili tuzo kwa ubunifu mkubwa uliotumika ndani ya video hii ambayo kwa sasa imeteka hisia na macho ya wafuatiliaji wa muziki wa Bongo Fleva Tanzania
https://youtu.be/j5f-61WZ3mk
Lonely - Marioo
Lonely ya Marioo haijawahi kuchuja tangu kuachiwa kwake na ndio maana mashabiki wameendelea kuifuatilia kwenye mitandaoni. Video ya wimbo huu imeongozwa na Director Kenny.
Utaniua - Zuchu
Utaniua ya Zuchu ni moja kati ya ngoma pendwa kwa sasa hasa video ya wimbo huo ambayo pia Diamond Platnumz anaonekana.
Leave your comment