TANZANIA: Diamond na Rick Ross Waingia Location Kuandaa Kitu Kipya

Msanii wa muziki nchini ambaye anafanya vizuri kimataifa, Diamond Platnumz Jumanne hii ameingia location kwaajili ya maandalizi ya kazi mpya akiwa na msanii mkubwa wa Hip Hip kutoka Marekani, Rick Ross.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo, Hallelujah ameonekana katika video na picha wakishoot Kazi hiyo ambayo haijajulikana ni kazi na namna gani.

Meneja wa kimataifa wa muimbaji huyo, Sallam amethibitisha kwamba wawili hao wameingia location kwaajili ya maandalizi ya Kazi hiyo.

“Diamond Platnumz x Rick Ross On set now somewhere in Miami #BlackBottleBoys and we never stop!!,” aliandika Instagram Sallam.

Rick Ross na Diamond wote ni mabalozi wa kinywaji cha Belaire ndio maana wanajiita BlackBottleBoys.

Source: bongo5.com

Leave your comment