Rose Muhando- 'Wanyamazishe Lyrics[Free Download]

[Photo Courtesy: Rose Muhando Instagram]

Wanyamazishe bwana
Milele wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakae kimya kimya

Wanyamazishe bwana
Wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakae kimya kabisa

Wapofushe macho yao
Wasinione wakae mbali nami
Ah wasinione

Kwa kuwa walitangaza msiba juu yangu
Wala hawakutaka ipone nafsi yangu
Wakafanya sherehe kupitia jina langu
Waliona fahari kutangaza mauti yangu
Wakachuma na pesa kupitia jina langu
Hawakuona vibaya kuumiza familia yangu
Walifanya dhihaka kudhihaki watoto wangu

Ah namtuma malaika nyumbani kwao
Atangaze msiba kwenye familia zao
Namtuma Gabrieli malangoni kwao
Atangaze msiba malangoni kwao

Nawafanye matanga maishani mwao
Natangaza msiba kwenye malango yao
Natangaza matanga nyumbani kwao
Yasikome matanga kwenye familia zao

Laana kifo, iwe juu yao
Wala wasiwe salama watoto wao
Mauti iwe fungu lao
Kushindwa uwe mbele yao
Kwa kuwa mimi nimekutumaini

Wanyamazishwe
Watahayarishwe, wafedheishwe
Wahangaike, waaibike
Kwa kuwa mimi nimekutumaini

Wanyamazishe bwana
Wafunge mpito kwa Yesu

Wanyamazishe bwana
Wafunge mpito kwa Yesu

Wapofushe macho yao
Wasinione wakae mbali nami
Ah wasinione

Ah Mikaeli wa vita namtuma kwao
Upeleke mafarakano kwao
Wasielewane waupwa wao
Nasema wagombane wao kwa wao

Walane watafunane wao kwa wao
Wavurugane wao kwa wao
Maadui wapigane wao kwa wao

Mungu mwenyezi awe adui wao
Wakitazama kulia wamwone Gabrieli
Wakitazama kushoto wamwone Micaeli
Mbele yangu wamwone Rafaeli

Wafadhaike
Watahayarishwe
wahangaishe
Wagonganishwe
Watayarike usiwape nafasi

Wanyamazishe bwana
Milele wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakimyee milele

Wanyamazishe bwana
Wanyamaze milele
Wafunge mpito kwa Yesu

Wapofushe macho yao
Wasinione wakae mbali nami
Ah wasinione

Wanyamazishe bwana
Wafunge mpito kwa Yesu
Wanyamazishe bwana
Wafunge mpito kwa Yesu
Wapofushe macho yao
Wasinione wakae mbali nami
Ah wasinione

https://www.youtube.com/watch?v=4nIfmZt71-4&list=PLnUFZ4sXj07gFmPL6C5UH5AxUAwJuwU7Q&index=2

Leave your comment