TANZANIA: Sijawahi kumsaliti Zari - Diamond

 

 

 

Msanii Diamond Platnumz alipokuwa kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio wiki kadhaa zilizopita alifunguka na kusema kuwa katika maisha yake toka ameanza kuwa na mahusiano na Zari hajawahi kumsaliti.

Diamond Platnumz anasema kuwa moja ya sababu kubwa kwa yeye kutomsaliti mpenzi wake huyo kwanza ni kwa sababu wanaonana mara kwa mara lakini kingine alidai kuwa kazi ya muziki siku zote inamfanya kuwa 'busy' kuhangaika na muziki hivyo hapati nafasi hiyo ya kuhisi anaweza kumsaliti mpenzi wake huyo.

"Mimi sijawahi kusaliti, kweli kabisa bado sijapangiwa nadhani lakini unajua mimi na Zari tunaonana mara kwa mara kwa kuwa nasafiri sana na huwa nina waambia watu kama Zari angekuwa anakaa Tanzania asingepata muda mzuri wa kukaa na mimi, kwa kuwa nasafiri sana kwa sababu za kikazi hivyo hata angekuwa Tanzania ningekuwa napishana naye, unajua masuala ya muziki yana stress sana kila siku unawaza nyimbo, unawaza video mara unatakiwa usimamie kazi za Harmonize atengeneze video kali, uhakikishe Rayvanny atengeneze ngoma kali mara Rich Mavoko aweze kuwa mkubwa zaidi kwa hiyo unakuwa kuna vitu vingi unavitazama hivyo unakosa muda wa mapenzi. Kwa mfano siku mbili nzima nimelala WCB sijalala nyumbani kwa ajili ya kazi za muziki." alisema Diamond Platnum

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

Leave your comment