TANZANIA: Goodluck Gozberth akanusha kuandika wimbo wa Rich Mavoko, Ibaki Story.

 

Producer, mwandishi wa nyimbo za Bongo Flava na muimbaji wa nyimbo za injili, Goodluck Gozbert ama kama anavyojulikana pia kama Lollypop, amekanusha kuandika wimbo wa Rich Mavoko, Ibaki Story.

 

 

Tetesi hizo zimekuwepo wiki hii na Rich tayari amezungumzia na kudai kuwa kuna vitu kadhaa Lollypop aliweka kwenye wimbo huo lakini si kwamba aliandika.

Akiongea na kipindi cha Super Mega cha Kings FM kinachoendeshwa na Divine Kweka, muimbaji huyo alisema:

"Mavoko tunafahamiana na tumewahi kuonana mara chache lakini kuhusu hiki kinachoendelea kutrend kwakweli sifahamu na tumewasiliana pia kuhusu hili akaniambia anashangaa, nikamuambia mimi pia nashangaa kuhusu hilo kwahiyo ni kitu ambacho sielewi kimetokana na nini na ni kwanini kinazungumzwa.”

“Ni tetesi tu na hazina ukweli wowote,” amesisitiza.

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

Leave your comment