TANZANIA: Namkubali sana Mr. Blue – Belle9

 

Msanii Belle nine amesema amkubali sana rapper Mr. Blue, kwani ni msanii ambaye amaeonyesha njia kwa vijana wengi kwa kitendo chake zha kuanza muziki akiwa mdogo.

Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Belle 9 amesema Mr. Blue ni rapper mzuri si kwa kuanza muziki akiwa mdogo, bali pia alishawahi kufanya naye kazi na kufanya vizuri.

 

 

“Mr. Blue ni rapper ninayemkubali alianza muziki akiwa na umri mdogo na kutuhamasisha wengi, hata nilipofanya naye kazi ya we ni wangu alifanya poa ni ikawa kazi nzuri”, alisema Belle 9.

Belle 9 ambaye ameachia remix ya wimbo wa 'burger, movie, selfie' amesema kuamua kushirikisha wasanii watano kwenye wimbo huo, ni idea aliyoipata baada ya watu wengi kumpigia simu kutaka remix au refix, na kaumua kuifanyia kazi mwenyewe kwa kuchanganya ladha tofauti tofauti.

“Unajua baada ya kuitoa burger, movie selfie, watu wengi walinipigia wanataka kufanya remix, cover, refix, nikaona niifanyie remx, na kuamua kuwashirikisha wasanii tofauti tofauti”, alisema Belle 9.

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

 

Leave your comment