TANZANIA: Ilikuwa ni issue ngumu sana kumshawishi Belle 9 ahamie Dar - Menejimenti

 

Uongozi wa kampuni ya Vitamin Music Group unaomsimamia Belle 9, umedai kuwa mtihani mkubwa uliokuwa nao ni kumshawishi Belle 9 ahamie Dar. Muimbaji huyo alihamia Dar mwaka jana baada ya kuendelea kuishi kwao Morogoro licha ya kuwa staa tayari.

Akiongea kwenye XXL cha Clouds FM wakati wa utambulisho wa remix ya Bulger Movie Selfie, meneja wake alidai kuwa ilibidi Belle ahamie Dar kutokana na kuwa kitovu cha burudani Tanzania.

“Ilikuwa ni issue ngumu sana kuweza kwasababu Belle 9 ana familia kule kwahiyo kumtoa Morogoro kumleta Dar ilikuwa ni issue kubwa sana,” alisema meneja wake.

Amesema uamuzi huo ulirahisisha mambo mengi. Belle ameachia remix ya Bulger Movie Selfie aliyowashirikisha Izzo B, G-Nako, Maua Sama, Jux na Mr Blue

 

Chanzo: Bongo5

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

Leave your comment