TANZANIA: Sina mahusiano na Ruby - Aslay

 

Msanii wa muziki wa bongo Rubby ambaye ameshirikishwa kwenye wimbo mpya wa kundi la Yamoto Band amefunguka na kusema yeye na Aslay si wapenzi kama ambavyo watu wanasema bali anadai hiyo ilikuwa ni njia kutangaza kazi yao mpya ambayo Rubby ameshiriki.

Kupitia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Rubby alidai ilibidi watafute kiki kuwa anatoka kimapenzi na Aslay ili waweze kuitangaza kazi hiyo mpya ya Yamoto Band inayoitwa 'Suu' ambayo wamefanya pamoja.

 

 

 

"Unajua siku hizi maisha yamebadilika na mashabiki wanapenda sana kiki, hivyo kwa kuwa wanapenda hayo ilibidi tuwape kitu roho inapenda lakini ukweli ni kwamba mimi na Aslay ni marafiki tu si wapenzi kabisa, ilikuwa kiki tu hiyo ili kusaidia kazi hii kufika sehemu kwa haraka" alisema Rubby

Kwa upande wake Aslay alipoulizwa juu ya suala hilo alisema kuwa kitu alichosema Rubby ndiyo uhalisia wenyewe na kukana si wapenzi kama ambavyo awali tetesi zilivyokuwa zikienea kwenye mitandao ambazo zilitengenezwa na wao wenyewe, kwa kuanza kupostiana kwenye mitandao ya kijamii.

 

Pakua app ya Mdundo sasa: smarturl.it/mdundo_ig_play_tz

 

 

Leave your comment