TANZANIA: Nisher alalamika kupoteza pesa nyingi kwenye video ya “Arosto”, na Gnako kuipotezea.

 

Muandaaji wa viideo nchini, Nisher alalamika kupoteza takriban shilingi milioni 3.9 kugharamia video ya wimbo wa G-Nako aliowashirikisha Nick wa Pili na Chin Bees uitwao ‘Arosto’ ambao Warawara anadaiwa kuipotezea baada ya kutoipenda.

Nisher amefafanunua kwa kina kwa kupost video Instagram baada ya kubaini kuwa G-Nako aliirudia video hiyo na Hanscana na kuiachia jana.

Nisher anahisi kilichofanyika ni kama usaliti kwake baada ya kuweka nguvu nyingi kwenye video hiyo aliyoitarajia imrudishe kwa kishindo. Anasema baada ya G-Nako kudai ‘hajatisha’ kwenye video hiyo na kwamba ‘ni ya kawaida sana’, Nisher alimuomba kama vipi atoe fedha ili warekebishe makosa hayo.

Anadai Warawara alisema hakuwa na hela ya kufanya hivyo muda huo. Kutokana na uamuzi wa G kuachia video aliyofanya na Hanscana, Nisher ameamua kuitoa yake pia ili kuwapa uhuru mashabiki wahukumu kama kweli video hiyo ni mbovu.

 

 

Tazama video zote mbili hapo chini, aliyoongoza Nisher na ile ya Hanscana.

Nisher:

Hascana:

 

 

Leave your comment