TANZANIA: Sitaki kolabo na mtu - Godzilla

 

 

Rapa Godzilla a.k.a King Zilla amesema hataki kolabo na mtu yoyote na taarifa ziwafikie kuwa kwa sasa anakuja na album mpya. Godzilla alifunguka alipoongea na eNews na kusema ana uwezo wa kufanya kazi zake mwenyewe bila msaada wa msanii mwingine, "Kwanini nipate usumbufu wa kumtafuta mtu wakati naweza kufanya kila kitu mwenyewe, hata chorus". Alisema King Zilla

Hii ni mara ya pili Godzilla anatoa shombo kuwa hahitaji kubebwa na mtu yoyote ili kumng'arisha kwenye game na kuwa ana plan ya kurudi "on top of the game", plan ambayo itaonekana zaidi kupitia album yake inayokuja soon.

 

Chanzo: Enews

 

 

Leave your comment