UGANDA: Aliyemuua Radio Aomba Msamaha

Kijana anayetuhumiwa kumuua msanii Mowzey Radio, Wamala Godfrey, ameomba msamaha kwa familia ya Radio pamoja na mashabiki, akisema kwamba tukio hilo alilifanya kwa bahati mbaya bila kukusudia.

Akiongea mahakamani nchini Uganda Wamala maarufu kama Troy amesema Radio alimteleza mikononi mwake na kuangukia sakafu, kitendo ambacho kilimuumiza vibaya kichwani na kupelekea kifo chake Februari 1, mwaka huu.

“Sikukusudia kumuua Mowzey Radio, aliniteleza tu kutoka mikononi mwangu na kwa bahati mbaya akapigiza kichwa chake kwenye sakafu , tafadhali nisamehe”, alisikika Troy mahakamani hapo.

Hata hivyo mahakama ya Uganda bado haijatoa hukumu ya kesi hiyo, ambayo imetokana na kifo cha msanii maarufu Afrika Mashariki Mosses Radio kwa kupigwa, mapema mwaka huu.

Courtesy: bongo5.com

Leave your comment