KENYA: Hizi Ndizo Nyimbo 3 Kutoka Afrika Mashariki Anazozikubali Akothee

Msanii Akothee amezitaja nyimbo tatu anazikubali na kuzisikiliza sana kutoka Afrika Mashariki.

Muimbaji huyo wa Kenya amezitaja nyimbo hizo ni Bado ya Harmonize, Thitima na Sitya Loss ya Eddy Kenzo kutoka Uganda.

“Kwanza kabisa ilikuwa ni ile ya Harmonize aliyomshirikisha Diamond, Bado. Hiyo nikishalewa tu kwenye kiti inakuwa kwenye playlist yangu inakuwa haiwezi kukosa,” Akothee amemuambia Mzazi Willy Tuva katika kipindi cha Msetoea cha Citizen Radio.

“Kwa hapa nyumbani kuna ile inaimbwa “Thitima”, unajua mimi sijuagi lyrics vizuri. Uganda kuna hii ngoma yakitambo lakini naipenda ile anaitwa nani huyu Eddy Kenzo ‘Sitya Loss’,” ameongeza.

Source: bongo5.com

Leave your comment