TANZANIA: Young Killer - Nawakubali sana Nikki Mbishi, Godzilah pamoja na marehemu Albert Mangwea kwa kufanya 'Free style.

 

 

Young Killer amefunguka na kusema hajawahi kumkubali rapa Fareed Kubanda  Fid Q kwenye kufanya mitindo huru kwa kuwa hajawahi kumuona mkali huyo wa hip hop Bongo akifanya mitindo huru. Young Killer alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema yeye anawakubali sana Nikki Mbishi, Godzilah pamoja na marehemu Albert Mangwea kwa kufanya 'Free style' sababu anatambua uwezo wao katika nyanja hiyo.

 

"Sijawahi kumkubali Fid Q kwa 'free style' sababu sijawahi kumuona akifanya hivyo ila niliowahi kuwaona wakifanya mitindo huru nampenda sana Nikki Mbishi, GodZillah pamoja marehemu Albert Magwea" alisema Young Killer.


Rapa Young Killer Msodoki ameweka wazi pia kuwa anatamani kufanya naye kazi kwa sasa ni Mbunge wa mikumi 'Prof Jay'."Kiukweli kabisa kwa sasa hivi mimi natamani sana kufanya kazi na Prof Jay, hata hivyo tayari nipo kwenye mipango ya kufanya kazi na rapper Chemical ". Aliongeza  Young Killer.
 

Leave your comment