TANZANIA: Rayvanny Amtaja Msanii Wake Mmoja wa TZ Ambaye Anatamani Kufanya Naye Kolabo

Msanii wa muziki kutoka WCB, Rayvanny amedai msanii wa kundi la Weusi Joh Makini ndiye msanii ambaye anatamani kufanya naye kolabo.

Akiongea na Bongo5 wiki hii, Rayvanny amedai bado hajazungumza na rapper huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Waya’.

“Bongo kuna wasanii wengi ambao ningependa kufanya nao kolabo lakini ukisema nimseme mmoja ambaye nawish ningefanya naye kitu ni Joh Makini,” alisema Rayvanny. “Joh namkubali sana na naona kama kuna kitu fulani chaajabu kitatokea nikifanya naye kolabo,”

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na kolabo ya wimbo ‘Kijuso’ aliyoshirikishwa na Queen Darleen, amedai bado hajafanya mazungumzo na Joh Makini kuhusu kolabo hiyo.

“Bado sijamwambia Joh Makini, lakini nadhani ukifika muda kila kitu kitafanyika. Kila kitu kitajulikana hapo lakini kama nikikutana naye nataka kufanya kitu tofauti sana,” alisema Rayvanny.

Source: bongo5.com

Leave your comment